Ijumaa, Julai 05, 2024

Karibu kwenye tovuti ya Jumuiya ya BUDECO!

BUDECO ni Shirika lisilo la kiserikali, kidini wala kikabila. Malengo yake yameainishwa katika Katiba ya jumuiya hii. Aidha asasi hii ilianzishwa tarehe 15/Oktoba/2013 kwa lengo la kuchangia shughuli za maendeleo, kuhamasiha na kuijengea uwezo jamii ya Wana-Busega ili kutumia rasilimali zilizopo kwa lengo la kuinua hali ya maisha ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni kama ilivyoainishwa katika dira, dhima na madhumuni ya katiba yake.

BUDECO inamilikiwa na kuendeshwa na Wanachama kupitia vyombo vyake. Lengo Kuu ni kuimarisha mshikamano na umoja miongoni mwa wanachama wake pamoja na wanachama wengine wa vyama vya kijamii nchini. Aidha BUDECO inaimarisha uhusiano mzuri baina ya Jamii ya Wanabusega waishio Busega na wale waihio nje ya Busega, pamoja na wafadhili mbalimbali wa asasi hii.

BUDECO mkutano wa pili 20140818 WA0011
Mwenyekiti wa BUDECO, Bw Maselle Joseph Ginhu akitoa taarifa kwenye mojawapo ya mikutano ya wanachama

BUDECO more pics from inauguration day
Wanachama wa umoja wa BUDECO wakisikiliza kwa makini yanayoendelea kwenye mkutano

BUDECO katika Elimu

BUDECO yachangia ujenzi wa madarasa Sh mil 34.7
icon siku ya makabidhiano ya mchango1

Chaki kutoka Maswa, Simiyu

WhatsApp group

Chat na wanaBUDECO papo kwa papo.
BUDECO chat
Tuma taarifa hizi zikiwa pamoja na namba yako ya simu na anuani ya email:
1.Majina yako matatu, 2.Kijiji unachotoka (kata na tarafa), 3. Kwa sasa unaishi wapi, 4. Shuguli unazofanya au unazopanga kufanya na makampuni/mashirika uliyofanyia/unayofanyia kazi (ukipenda lakini)

Tuma kwenye namba hii 0713-982855 na baadaye ukumbini kwa kujitambulisha.