Wednesday, July 03, 2024

RM, 01/03/2018
Jumuiya ya Maendeleo ya Wana-Busega waishio nje ya Busega, BUDECO (Busega Development Community) imepongezwa na mkuu wa wilaya ya Busega Bi. Tano Seif Mwera kwa kutoa mchango wa fedha taslimu Shilingi 34,700,000/= kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika wilaya ya Busega.

Mchango huu uliwasilishwa rasmi siku ya Jumatatu tarehe 26/02/2018 katika ofisi ya mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa Jumuiya ya BUDECO Bw. Maselle Joseph Ginhu kwa kushirikiana na mwakilishi wa wanachana waishio karibu na Busega, Dr. Simon Songe. 

siku ya makabidhiano ya mchango5 mkuu wa wilaya bi tano akimkabidhi mkiti maselle hati
Mkuu wa wilaya ya Busega Bi. Tano Mwera akimkabidhi hati ya shukurani Mwenyetiki wa BUDECO Bw. Maselle Joseph Ginhu. Aliyesimama katikati ni Dr Simon Songe.

Katika hafla hiyo fupi ya makabidhiano ya mchango huu ambayo ilishuhudiwa pia na viongozi mbalimbali wa wilaya ya Busega, mkuu wa wilaya Bi. Tano Mwera alinukuliwa akisema:
“Kwa niaba ya wilaya ya Busega nawashukuru sana wana-BUDECO kwa mchango huu wa kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika wilaya yetu ya Busega.”

Aliendelea kwa kuwahimiza wadau wengine kuona umuhimu wa kuchangia sekta ya elimu ili kutatua changamoto ya miundombinu iliyopo katika shule za msingi na za sekondari. Akiahidi kusimamia vizuri matumizi ya mchango huu alisema:  “Natumia nafasi hii pia kuahidi michango hii tutaifuatilia na kuisimamia kwa karibu sana ili kuhakikisha kwamba inatumika vizuri kwa ujenzi kama ilivyokusudiwa ili kuweza kuwanufaisha wanaBusega na Watanzania kwa ujumla.”

Akikabidhi msaada huu, mwenyekiti wa BUDECO -- Jumuiya ya Maendeleo ya Wana-Busega -- Bw. Maselle Joseph Ginhu alisema; Kwa kutokana na changamoto zinazoikabili sekta ya elimu katika Wilaya ya Busega, wanachama wa BUDECO waliamua kukaa kikao na kuchangishana na kisha kupata kiasi hicho cha fedha ili kuwaokoa wanafunzi waliobaki nyumbani kwa kukosa vyumba vya madarasa. Bwana Ginhu alinukuliwa akisema: “Sisi wanaBusega tuishio nje ya Busega tuliguswa na hilo, hivyo tukaamua  kuchangishana. Tumeweza kukusanya shilingi milioni 34.7 ambazo leo tumezikabidhi kwenye ofisi ya wilaya na mbele ya viongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Busega ili ziweze kwenda kutekeleza ujenzi wa hayo madarasa ambayo yalikuwa yamekwamisha wanafunzi.”

siku ya makabidhiano ya mchango2 mkiti maselle akitambulisha budeco
Mwenyekiti wa jumuiya ya WanaBusega Bw. Masele akifafanua shughuli za BUDECO kwa viongozi wa wilaya ya Busega

Itakumbukwa kuwa wilaya ya Busega ni miongoni mwa wilaya zilizofanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka jana (2017) katika mkoa wa Simiyu, lakini bado kuna idadi kubwa ya wanafundi ambao hawajajiunga na kidato cha kwanza kwa kutokana na changamoto za miundombinu hususani upungufu wa vyumba vya madarasa.

Mchango huu kwa ajili ya ujenzi wa madarasa wilayani Busega ni baadhi tu ya shughuli za kimaendeleo zinazofanywa na jumuiya ya BUDECO (Busega Development Community). Aidha BUDECO ni shirika lisilo la kiserikali, kidini wala kikabila. Malengo yake yameainishwa vizuri katika Katiba ya shirika hili, hususani katika maelezo ya dira, dhima na madhumuni yake kwamba ilisajiliwa rasmi tarehe 15/Oktoba/2013 kwa lengo la kuchangia shughuli za Maendeleo, kuhamasisha na kuijengea uwezo jamii ya WanaBusega ili kutumia rasilimali zilizopo kwa lengo la kuinua hali ya maisha ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.

Kwa maelezo zaidi tafadhali tembelea tovuti rasmi ya jumuiya hii   www.budeco.co.tz    

# Video ya makabidhiano ya mchango wa ujenzi wa miundombinu ya shule katika wilaya ya Busega:

WebM media format: Makabidhiano ya mchango wa ujenzi wa madarasa wilaya ya Busega

# Picha nyinginezo za makabidhiano ya mchango wa ujenzi wa madarasa katika wilaya ya Busega:

Mwenyekiti wa BUDECO Bw. Ginhu akitoa maelezo ya jumuiya

Mwenyekiti wa BUDECO Bw. Ginhu akitoa maelezo ya jumuiya

Ujenzi wa madarasa ukiendelea wilayani Busega

Ujenzi wa madarasa ukiendelea wilayani Busega

Mkuu wa wilaya akimkabidhi mwenyekiti wa BUDECO Bw. Ginhu hati ya shukurani

Mkuu wa wilaya akimkabidhi mwenyekiti wa BUDECO Bw. Ginhu hati ya shukurani

Mwenyekiti wa BUDECO Bw. Ginhu akipongezwa na Mh Diwani Luyenze

Mwenyekiti wa BUDECO Bw. Ginhu akipongezwa na Mh Diwani Luyenze

Hati ya shukurani ya mchango wa elimu kwa jumuiya ya BUDECO

Hati ya shukurani ya mchango wa elimu kwa jumuiya ya BUDECO

Makabidhiano ya mchango wa BUDECO kwa mkuu wa wilaya

Makabidhiano ya mchango wa BUDECO kwa mkuu wa wilaya

Wanafunzi wilayani Busega wakisoma kwa bidii

Wanafunzi wilayani Busega wakisoma kwa bidii

Wanachama wa BUDECO na viongozi wa halmashauri

Wanachama wa BUDECO na viongozi wa halmashauri


___
Maelezo ya ziada kwenye makala haya na video yametoka kwa:
Bw. Shaban Lupimo (StarTV) na Bw. Joel Shushu (Magazeti ya serikali)

BUDECO katika Elimu

BUDECO yachangia ujenzi wa madarasa Sh mil 34.7
icon siku ya makabidhiano ya mchango1

Chaki kutoka Maswa, Simiyu

WhatsApp group

Chat na wanaBUDECO papo kwa papo.
BUDECO chat
Tuma taarifa hizi zikiwa pamoja na namba yako ya simu na anuani ya email:
1.Majina yako matatu, 2.Kijiji unachotoka (kata na tarafa), 3. Kwa sasa unaishi wapi, 4. Shuguli unazofanya au unazopanga kufanya na makampuni/mashirika uliyofanyia/unayofanyia kazi (ukipenda lakini)

Tuma kwenye namba hii 0713-982855 na baadaye ukumbini kwa kujitambulisha.