BUDECO is a non-governmental, non-religious and non-tribal organization with its mission outlined in its constitution. The organization was established on the 13th of October 2013 with the aim of stimulating developments and building capacity to the Busega community to use available resources for improving their social, economic, and cultural welfare as outlined in vision, mission, and objectives of its constitution.
Read more ...
Dar es Salaam, 26/Oktoba/2019
Uongozi wa BUDECO leo hii ukiwakilishwa na Naibu Mwenyekiti Bwana Mashauri Nkonoki na Mtunza Hazina Dr Julius Manyanda na Bwana Mathias Lung'wecha wameshiriki kwenye hafla iliyoandaliwa na Baraza la Mitihani Jijini Dar-es-Salaam, Mlimani City, kwa ajili ya kuwatunuku wanafunzi waliofanya vizuri kwenye mtihani wa darasa la saba 2019.
Aidha uongozi wa BUDECO, shirika ambalo ni miongoni mwa wadau wakubwa wa elimu katika wilaya ya Busega mkoani Simiyu umewapongeza sana wanafunzi wane (4) – wavulana watatu na msichana mmoja -- walioshika nafasi muhimu ndani ya kumi (10) bora kitaifa, waalimu, wazazi na uongozi wote wa wilaya kwa kuwezesha ufaulu huu.
-- PICHA Wanafunzi wa Busega walioingia kwenye 10 bora kitaifa wakiwa na viongozi wa wilaya jijini Dar es Salaam --
Mheshimiwa mbunge wa Busega, Dr Raphael Chegeni alinukuliwa akisema: “Ni faraja kubwa kwa wana Busega wote ikiwa ni historia kwa ufaulu wa vijana wetu waliomaliza darasa la saba. Kitaifa matokeo yametupa uwepo wa vijana wetu kwenye nafasi muhimu za kitaifa. Napenda kuwapongeza sana wanafunzi hawa walioshika nafasi muhimu ndani ya 10 bora kitaifa, waalimu, wazazi na uongozi wote wa wilaya kwa kuwezesha ufaulu huu. Tunataraji hata vijana wetu wa kidato cha nne nao watafanya vizuri.”
Read more ...
Wana-BUDECO, Wana-Busega na Watanzania kwa ujumla tumepokea kwa masikitiko makubwa sana kifo cha kijana wetu, Bw. Nelson V. Mabeyo na abiria wengine kilichotokea katika ajali ya ndege huko Seronera hapo Jumatatu, tarehe 23/09/2019.
(c) www.thecitizen.co.tz
Bwana awape faraja familia ya mkuu wa majeshi Tanzania, CDF Venance Mabeyo, ndugu, marafiki na jamaa wote kwa msiba huu mzito.
Kijana wetu mpendwa, mtoto wa mwanachama mwenzetu wa BUDECO, umeondoka wakati taifa zima la Tanzania linakutegemea na lina uhitaji wa taaluma yako na uwepo wako.
Wana BUDECO tunaendelea na mipango ya kushiriki kikamilifu kwa kuwafariji wafiwa katika msimba huu.
Tunaomba Mwenyezi Mungu awape ustahimivu na faraja ya Moyo.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
RIP NELSON V. MABEYO. AMINA.
PS:
MCHANGO WA RAMBIRAMBI KWA NDG CDF VENANCE MABEYO ALIYEFIWA NA MTOTO WAKE ITUMWE KWA MPESA, AIRTEL MONEY AU TiGO PESA kwa kutumia namba hizi: 0752 845 357 au 0712 291 400. Majina ya namba hizo ni Mashauri Kanesenese.
Asanteni.
Mwenyetiki wa BUDECO
Bw. Maselle Joseph Ginhu
Read more ...
RM, 01/03/2018
Jumuiya ya Maendeleo ya Wana-Busega waishio nje ya Busega, BUDECO (Busega Development Community) imepongezwa na mkuu wa wilaya ya Busega Bi. Tano Seif Mwera kwa kutoa mchango wa fedha taslimu Shilingi 34,700,000/= kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika wilaya ya Busega.
Mchango huu uliwasilishwa rasmi siku ya Jumatatu tarehe 26/02/2018 katika ofisi ya mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa Jumuiya ya BUDECO Bw. Maselle Joseph Ginhu kwa kushirikiana na mwakilishi wa wanachana waishio karibu na Busega, Dr. Simon Songe.
Mkuu wa wilaya ya Busega Bi. Tano Mwera akimkabidhi hati ya shukurani Mwenyetiki wa BUDECO Bw. Maselle Joseph Ginhu. Aliyesimama katikati ni Dr Simon Songe.
Katika hafla hiyo fupi ya makabidhiano ya mchango huu ambayo ilishuhudiwa pia na viongozi mbalimbali wa wilaya ya Busega, mkuu wa wilaya Bi. Tano Mwera alinukuliwa akisema:
“Kwa niaba ya wilaya ya Busega nawashukuru sana wana-BUDECO kwa mchango huu wa kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika wilaya yetu ya Busega.”
Read more ...
On 12/09/2014 the Busega Development Community organisation (BUDECO) condemned vehemently the rape incident, which occured in Busega district, in Simiyu region on 23/08/2014.
A group of gansters invaded the house of Mr. Samwel Mkumbo at night, where they robbed 18 milion Shilings and later on went on to attack a young teacher in her room within the compound. The teacher was robbed about 50,000 Shillings and raped by the group of men.
While reading the statement of BUDECO during a press conference in Dar es Salaam on 12/09/2014, the chairman of BUDECO, Mr. Ginhu Joseph Masele said, this rape incident must be condemned vehemently by everyone as it will negatively affect the education sector, which is among the main challenges in the district.
Read more ...